STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 19, 2010

Dady, J-Mupa wote pamoja



WASANII wanaokuja juu kwenye muziki wa kizazi kipya ambao kila mmoja anatamba na kibao chake, Leonard Fidelis 'Dady' na Juma Mussa 'J-Mupa' wanajiandaa kutoa albamu ya pamoja ya nyimbo 16.
Wakizungumza na Micharazo, wasanii hao, walisema albamu hiyo ya pamoja itakuwa na mchanganyiko wa miondoko tofauti ya R&B, Ragga na Hip Hop.
Dady anayetamba na kibao cha 'Ni Gani', alisema ana uhakika hiyo ya pamoja itawaweka kwenye matawi ya juu, kutokana na ukweli kwamba muda mrefu wamekuwa wakijitahidi kutoka bila mafanikio.
Lakini sasa wameangukia mikononi mwa meneja wao mpya waliyemtaja kwa jina la Nassa na kwamba wana imani atasaidia kuhakikisha wanatoka upya na tena kwa kishindo.
"Baada ya kusota kitambo, hatimaye nimeachia kazi mpya iitwayo Ni Gani, huku nikiwa katika maandalizi ya kutoa albamu pamoja na mshirika wangu, J-Mupa, tutakayeshea nyimbo 16," alisema.
Dady alisema baadhi ya nyimbo zilizomo kwenye albamu hiyo ya pamoja ni kibao chao cha pamoja walichokitoa mwaka 2006 cha 'Uvumilivu', 'Upungufu', 'Inatosha', 'Rudi', 'Ni Gani', 'Namsaka' na nyinginezo.
Kwa upande wake J Mupa, anayetamba na 'Mzuri Yupi', alisema albamu yao hiyo huenda ikaleta mapinduzi kutokana na jinsi wanavyoumiza kichwa kuiandaa.
"Ni albamu bab' kubwa muhimu ni wapenzi na mashabiki kutupa sapoti ya kutosha ili tufanikiwe kutoka na kuwapa burudani murua," alisema J-Mupa ambaye pia hujihusisha na masuala ya filamu.

No comments:

Post a Comment