STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 19, 2010

Matumla adundwa na Maugo, astaafu ngumi






BINGWA wa zamani wa Dunia wa ngumi za kulipwa, Rashid Matumla 'Snake Boy' jana alipigwa kwa pointi na Mada Maugo na kutangaza kustaafu kuendelea kupigana na ulingoni na badala yake kugeukia kazi ya ukocha.
Pambano hilo lililoandaliwa na Oganizesheni ya Ngumi za Kulipwa nchini, TPBO, lilifanyika kwenye ukumbi wa PTA, Sabasaba Dar es Salaam kwa nia ya kumaliza ubishi baina ya wawili hao waliokuwa wakitambiana kwa muda mrefu.
Matumla ambaye alishawahi kutangaza kuacha ngumi baada ya kupigwa kwa mara nyingine na Francis Cheka 'SMG', alishindwa kuhimili vishindo vya Maugo, ingawa alimudu hadi mwisho wa mchezo huo uliokuwa wa raundi 10 uzito wa kilo 72.
Mara baada ya kumalizika kwa pambano hilo lililotanguliwa na michezo kadshaa ya utangulizi, Snake Boy, alitangaza kuwa huo ndio mchezo wake wa mwisho kupanda ulingoni na kwamba anaamini 'ameshazeeka' na kusema atageukia ukocha ili kuwarithisha vijana ujuzi wake wa mchezo huo uliompa sifa kubwa ndani na nje ya nchi.
Kutokana na ushindi huo wa pointi, Mada Maugo sasa anaweza kupigana na Cheka, ambaye alishatangaza kama bondia huyo atashinda basi atakuwa radhi kupigana nae au la yeye (Cheka) atamtafuta Karama Nyalawila ili kumaliza ubishi baada ya wawili hao yaani Maugo na Nyalawila kutamba kuwa ndio pekee wanaoweza kumsimamisha Cheka.

No comments:

Post a Comment