STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 27, 2010

Cheka amlaumu meneja wake

BINGWA wa dunia wa ngumi za kulipwa anayetambuliwa na mashirikisho ya ICB na UBO Francis Cheka amemlaumu meneja wake Juma Ndambile kwa kushindwa kumuandalia mapambano. Aidha, amedai anajuta kuingia nae mkataba ambao "unamfunga" bila faida.
Akizungumza na Micharazo, Cheka alisema katika kipindi cha mwaka mmoja alioingia mkataba na meneja huyo, ameshakosa michezo kadhaa ikiwemo pambano la kimataifa lililokuwa lifanyike Uingereza pamoja na mengine ya ndani.
Cheka, alisema hajui ni kwa nini meneja huyo anashindwa kumsaidia katika hilo wakati anatambua kuishi kwake kunategemea ngumi.
"Kwa kweli huwa najuta kwa nini niliingia mkataba na meneja huyu kwa jinsi anavyonizibia riziki zangu wakati hanitafutii mapambano ya kuniwezesha kuingiza fedha na pia kupima kiwango changu," alisema Cheka.
Aliongeza kuwa hata suala la malipo ya mishahara aliyokubaliana naye imekuwa ikilegalega na kusisitiza huenda asiongeze mkataba mpya na meneja huyo mara mkataba wa sasa utakapomaliza Desemba mwaka huu.
Hata hivyo Ndambile alisema madai ya Cheka ni ya "kitoto" kwa sababu yeye ni meneja na sio promota.
Wakati akiingia mkataba na bondia huyo alimlipa mishahara ya muda wa miezi sita pamoja na fedha nyingine za ziada kwa ajili ya dharura, alisema Ndambile.
Aliasema alimlipa mishahara ya miezi sita ambayo ni shilingi milioni 1.2 na kumpa dola za kimarekani 1,500 za maandalizi ya michezo atakayoipata na hivyo kushangazwa na tuhuma kwamba anamzungumza kumlipa chake.
"Anachokisema ni utoto, mimi sio promota ni meneja wake na unajua kazi za umeneja, hivyo sijui anataka nimfanyie nini," alisema Ndambile.
"Pia amekuwa akipata mapambano kibao, lakini amekuwa akiyakwepa kiasi cha kuwakera hata wadhamini waliojitolea kwa ajili yake."
Alisema bado anaendelea kumtambua Cheka kama bondia wake na ataendelea kumsimamia atakapopata mapambano kama mkataba unavyojieleza.

No comments:

Post a Comment