STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 27, 2010

Wanamichezo wauota ubunge 2010

MWENYEKITI wa klabu ya Simba, Ismail Rage anaongoza orodha ya wanamichezo waliojitosa kwenye mchakato wa kuwania kuteuliwa kuwa wagombea na viti vya ubunge katika uchaguzi mkuu ujao wa Oktoba 31.
Rage anawania jimbo la Tabora Mjini kwa tiketi ya CCM, ambalo linashikiliwa kwa sasa na Juma Kaboyoga ambaye anakitetea kiti hicho.
Wanamichezo wengine wanaotaka ubunge ni pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mchezo Netiboli, CHANETA, Shy Rose Bhanji anayewania Jimbo la Kinondoni, Seneta wa zamani wa Yanga, Nasor Duduma na Mwenyekiti aliyemaliza muda wake katika klabu hiyo Imani Madega wao wamejitosa kwenye mbio hizo wakiwania Jimbo la Chalinze.
Wengine ni aliyekuwa Katibu Mkuu wa TFF, Frrdirick Mwakalebela, aliyejitosa jimbo la Iringa Mjini, mkimbiaji bingwa wa zamani, John Bura aliyejitosa Jimbo la Karatu, Mkurugenzi wa Simba, Aziz Aboud aliyeomba katika jimbi la Morogoro Mjini.
Phares Magese, Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho la Kikapu nchini, TBF, aliyejitosa Jimbo la Kigamboni.
Pia katika kinyang'anyiro hicho cha mbio za siasa, Mtangazaji wa Mtangazaji wa Channel Ten, Cyprian Msiba amejitosa Jimbo la Mwibara.
Majina ya wagombea wateule wa viti vya ubunge ndani ya CCM yanatarajiwa kutangazwa Agosti 1 baada ya kukamilika kwa kura za maoni za wanachama wa chama hicho.

No comments:

Post a Comment