STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 27, 2010

Rais wa Tandale aja na filamu ya Mbagala


=============================


KIBAO cha 'Kwetu Mbagala' kinachozidi kutamba nchini cha msanii Naseeb Abdul 'Diamond' a.k.a 'Rais wa Tandale' kinatarajiwa kutengenezewa filamu itakayopewa jina hilo hilo la 'Mbagala'.
Akizungumza na Blog hii, Diamond, alisema tayari ameshaanza maandalizi ya kufyatua filamu hiyo ambayo itawashirikisha wasanii nyota wa fani hiyo akiwemo Jacqueline Wolper.
Diamond alisema lengo la kutoa filamu hiyo ni kutaka kufafanua ukweli juu ya kibao chake ambacho kimekuwa kikilalamikiwa na baadhi ya wapenzi na mashabiki wa fani hiyo wakazi wa eneo hilo la jijini wakidai amewadhalilisha.
"Baada ya kibao changu cha 'Mbagala' kutamba, natarajia kuja na filamu yenye jina hilo ambayo itawashirikisha wasanii kadhaa nyota, akiwemo Wolper, mimi mwenyewe na wengineo ambao wataifanya iwe ya kiwango," alisema Diamond.
Aliongeza kuwa kutoka kwa filamu hiyo kutamaliza 'ubishi' juu ya ukweli kama kibao chake cha 'Mbagala' kilikuwa kinalenga kuwadhalilisha wakazi wa Mbagala au alitumia jina hilo kupata vina vya wimbo huo, ilihali alikuwa akilenga maskani yake ya Tandale alipokulia.
"Mengi yamesemwa juu ya kibao hiki, lakini itakapotoka filamu yake ndio watu watajua mimi sikuwa na nia mbaya ya kusanifu kitongoji hicho, ila nililazimika kutumia jina lake kufikisha ujumbe juu ya mkasa wa kimapenzi na eneo letu nililokulia la Tandale," alisema

No comments:

Post a Comment