STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, July 7, 2010

Forlan alicheza akiwa majeruhi-Kocha




CAPE TOWN, Afrika Kusini
NYOTA tegemeo wa timu ya taifa ya Uruguay, Diego Forlan, alicheza pambano la nusu fainali dhidi ya Uholanzi akiwa majeruhi na kumlazimisha kocha wake Oscar Tabarez, kumtoa nje kabla ya kumalizika kwa pambano hilo.
Forlan aliyekaririwa jumanne iliyopita kwamba katu hawezi kurejea tena katika Ligi Kuu ya Uingereza na kufuta ndoto za meneja wa Tottenham Hotspur, Harry Redknapp kumnyakua, alimua tangu mwanzo wa mchezo huo.
"Tangu dakika ya kwanza Forlan alikuwa na tatizo. Aliumia na hakuweza kuendelea kucheza,"
"Alikuwa na maumivu na wakati wa mchezo tuliamua kuchukua maamuzi ya kumjaribu kumbadili na mchezaji mwingine" aliongeza Tabarez.
Hata hivyo kocha huyo alisema tatizo la mshambuliaji huyo anayeichezea Atletico Madrid ya Hispania, sio kubwa na huenda kesho akacheza kuipigania nchi yake katika pambano la kusaka mshindi wa tatu kati yao na mshindi kati ya Ujerumani na Hispania.
"Sio tatizo lake halikuwa kubwa, lakini hakuwa fiti kwa asilimia 100 kucheza hadi mwisho," alisema kocha huyo.
Forlan, mshambuliaji wa Atletico Madrid ya Hispania, alifunga bao maridadi wakati timu yake iliposhindwa mabao 3-2 na Uholanzi.
Mshambuliaji huyo alifunga bao hilo dakika moja kabla ya mapumziko kwa shuti kali la umbali ya mita 30 lililomshinda nguvu kipa wa Uholanzi, Maarten Stekelenburg.
Huenda kesho mchezaji huyo aliyeifungia timu hiyo mabao manne katika fainali hizo za WOZA 2010 akawemo katika pambano la kusaka mshindi wa tatu litakalochezwa kwenye mjini wa Port Elizabeth.

No comments:

Post a Comment