STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, January 7, 2014

Chelsea vs Stoke City, Arsena vs Covenrry City FA Cup

LONDON, England
IKIWA katika moto mkali vinara wa Ligi Kuu ya England Arsenal itawakabili Coventry City inayoshiriki Ligi Daraja la pili katika raundi ya nne ya Kombe la FA, huku Chelsea wakipangiwa kuvaana na Stoke City.
Arsenal iliwatoa  mahasimu wao wa mji wa London, Tottenham Jumamosi  na sasa itaavana na Coventry  na kutoa tumaini kwa timu hiyo kupenya kirahisi baada ya kulitwaa taji hilo mara ya mwisho mwaka 2005.
Mwkaa jana katika michuano hiyo Arsenal ilitolewa kwenye raundi ya tano na Blackburn Rovers na hivyo ni nafasi yao ya kuvuka hatua hiyo kuendea mafanikio ya mwaka 2005 ilipotwaa taji hilo, huku pia ikiwa katika mbio za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu iliyopata kwa mara ya mwisho zaidi ya misimu mitano iliyopita.
Chelsea watawakaribisha Stoke, wakati Manchester City watacheza dhidi ya Bristol City ama Watford kama watawang'oa Blackburn katika mechi yao ya marudiano kwenye Uwanja wa Etihad baada ya kutoka sare ya 1-1 Jumamosi ugenini.
Mechi za raundi ya nne zitapigwa Januari 25 na 26.
Zawadi ya Swansea kwa kuwatoa Manchester United kwenye Uwanja wa Old Trafford juzi ni safari ya ugenini dhidi ya timu ya daraja la kwanza ya Birmingham City, Bristol Rovers ya daraja la tatu ama Crawley ya daraja la kwanza - kwani timu hizo mbili za mwisho hazijacheza mechi yao ya marudiano iliyoahirishwa.
Mabingwa watetezi Wigan watawakaribisha Crystal Palace kama watawafunga MK Dons katika mechi yao ya marudiano baada ya timu hizo mbili kutoka sare ya 3-3 Jumamosi.
Kikosi cha kocha Roberto Martinez cha Everton kitaenda kuikabili timu ya daraja la pili ya Stevenage, wakati Cardiff ya kocha Ole Gunnar Solskjaer itasafiri kwenda kucheza na timu ya daraja la kwanza ya Bolton Wanderers.
Liverpool, ambao waliifunga timu ya daraja la pili Oldham 2-0 Jumapili, watasafiri kuwakabili kati ya timu ya daraja la kwanza ya Bournemouth ya daraja la tatu ya Burton.
Hull City watasafiri kuivaa timu ya daraja la tatu ya Southend, ambayo inafundishwa na kocha wa zamani wa Hull, Phil Brown.
Timu mbili za "mchangani" bado zimo katika michuano hiyo, lakini zitahitaji kushinda mechi zao za marudiano za raundi ya tatu ili kuingia raundi ya nne.

RATIBA RAUNDI YA NNE:
Sunderland v Kidderminster or Peterborough
Bolton v Cardiff
Southampton v Yeovil
Huddersfield v Charlton or Oxford
Port Vale or Plymouth v Brighton
Nottingham Forest v Ipswich or Preston
Southend v Hull
Arsenal v Coventry
Stevenage v Everton
Wigan or MK Dons v Crystal Palace
Chelsea v Stoke
Blackburn or Manchester City v Bristol City or Watford
Bournemouth or Burton v Liverpool
Birmingham, Bristol Rovers or Crawley v Swansea
Sheffield United v Norwich or Fulham

No comments:

Post a Comment