STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 8, 2014

Mashetani Wekundu wadundwa tena

Namanja Vidic akishangilia bao lake la kusawazisha la Man Utd ambalo hata hivyo halikusaidia kitu
MANCHESTER United imeendelea kuwa 'mdebwedo' chini ya kocha David Moyes baada ya usiku wa jana kulambishwa tena kipigo cha 2-1 na Sunderland katika mechi ya kwanza ya Nusu Fainali ya Kombe la Ligi.
Mashetani hao Wekundu walikumbana na kipigo hicho ugenini na kuzidi kumweka pabaya Moyes aliyeichukua timu hiyo toka mikononi mwa kocha aliyekuwa na mafanikio makubwa Old Trafford, Alex Ferguson.
Sunderland ikiwa kwenye uwanja wake wa Uwanja wa Light ilijikuta ikizawadiwa bao dakika za nyongeza baa da mkongwe Ryan Giggs kujifunga.
Kipindi cha pili kilianza kwa Manchester kufanikiwa kusawazisha bao hilo dakika ya 52 kupitia kwa nahodha wake, Nimanja Vidic hata hivyo wenyeji waliwakata maini wageni wao baada ya Borini kufunga bao la ushindi kwenye dakika ya 65 kwa mkwaju wa penati.

No comments:

Post a Comment