STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 1, 2016

Rashford naye ndani katika kikosi cha mwisho cha England

http://img.thesun.co.uk/aidemitlum/archive/02717/04_01125924_ff23d4_2717346a.jpgLAZIMA iwashike. England imetangaza kikosi chake cha wachezaji 23 kwa ajili ya michuano ya Fainali za UEFA Euro 2016, huku chipukizi wa Manchester Utd, Marcus Rashford akijumuishwa katika kikosi hicho.
Rashford mwenye umri wa miaka 18, alifunga bao katika mechi yake ya kwanza ya kimataifa wakati Uingereza waliposhinda mabao 2-1 dhidi ya Australia katika mchezo wa kirafiki uliofanyika Ijumaa iliyopita. Mshambuliaji wa Liverpool Daniel Sturridge naye pia amejumuishwa, lakini Andros Townsend wa Newcastle Utd na Danny Drinkwater wa Leicester City wote wameachwa katika kikosi hicho cha mwisho chini ya Kocha Roy Hodgson. 
England inatarajiwa kuchuana na Ureno katika mchezo wa kujipima nguvu kabla ya kuanza kwa michuano hiyo ikishuka dimbani siku moja baada ya uzinduzi wa michuano hiyo inayaofanyika Ufaransa.
England itaanza kibarua chake Juni 11 kwa kuvaana na Urusi. 
Kikosi kamili cha Three Lions ni kama ifuatavyo;
Makipa: Joe Hart (Manchester City), Fraser Forster (Southampton), Tom Heaton (Burnley). 
Mabeki: Gary Cahill (Chelsea), Chris Smalling (Manchester United), John Stones (Everton), Kyle Walker (Tottenham Hotspur), Ryan Bertrand (Southampton), Danny Rose (Tottenham Hotspur), Nathaniel Clyne (Liverpool). 
Viungo: Dele Alli (Tottenham Hotspur), Ross Barkley (Everton), Eric Dier (Tottenham Hotspur), Jordan Henderson (Liverpool), Adam Lallana (Liverpool), James Milner (Liverpool), Raheem Sterling (Manchester City), Jack Wilshere (Arsenal). Washambuliaji: Wayne Rooney (Manchester United), Harry Kane (Tottenham Hotspur), Jamie Vardy (Leicester City), Daniel Sturridge (Liverpool), Marcus Rashford (Manchester United).

No comments:

Post a Comment