STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 1, 2016

Maskini Marco Reus aachwa tena Ujerumani

http://img.bleacherreport.net/img/images/photos/002/728/809/hi-res-450616209-marco-reus-of-germany-in-action-during-the_crop_exact.jpg?w=1500&h=1500&q=85SIJUI ni mikosi au basi tu. Kocha wa timu ya taifa ya Ujerumani, Joachim Low amemuacha mshambuliaji wa Borussia Dortmund Marco Reus katika kikosi chake cha mwisho cha wachezaji 23 kwa ajili ya michuano ya Euro 2016.
Kocha Low alitangaza kikosi chake huku mbali na kumuacha Reus lakini pia amewaacha Karim Bellarabi na Julian Brandt wa Bayer Leverkusen na Sebastian Rudy wa Hoffenheim.
Nyota hao wanne sasa wanatarajiwa kuondoka katika kambi ya timu hiyo huko Uswisi.
Ujerumani itacheza mechi yake ya mwisho ya kujipima nguvu dhidi ya Hungary kabla ya kucheza mechi yao ya ufunguzi wa michuano ya Euro 2016 dhidi ya Ukraine. Reus alishindwa kusalia kwenye kikosi cha Mabingwa hao wa Dunia katika fainali za Kombe la Dunia za mwaka juzi nchini Brazili, badala ya kuumia, lakini safari hii yupo fiti, lakini kafungiwa vioo.
Kikosi kamili:

Makipa: Manuel Neuer (Bayern Munich), Bernd Leno (Bayer Leverkusen), Marc-Andre ter Stegen (Barcelona).

Mabeki: Jerome Boateng (Bayern Munich), Emre Can (Liverpool), Jonas Hector (Cologne), Benedikt Howedes (Schalke), Mats Hummels (Borussia Dortmund), Shkodran Mustafi (Valencia), Antonio Rudiger (Roma).
Viungo: Julian Draxler (Wolfsburg), Mario Gotze (Bayern Munich), Sami Khedira (Juventus), Joshua Kimmich (Bayern Munich), Toni Kroos (Real Madrid), Mesut Ozil (Arsenal), Leroy Sane (Schalke), Bastian Schweinsteiger (Manchester United), Julian Weigl (Borussia Dortmund).

Mastraika: Mario Gomez (Besiktas), Thomas Muller (Bayern Munich), Lukas Podolski (Galatasaray), Andre Schurrle (Wolfsburg).

No comments:

Post a Comment