STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 7, 2016

Bocco, Mao waomba radhi Azam kuchemsha Mapinduzi Cup


http://cecafafootball.org/wp-content/uploads/2014/03/john-bocco.jpg
John Bocco
Kikosi cha Azam kilichotolewa Mapinduzi Cup jioni ya leo visiwani Zanzibar

NAHODHA wa Azam, John Bocco 'Adebayor' amewaomba radhi mashabiki na wapenzi wa klabu hiyo kwa matokeo mabaya ambayo timu hiyo imeyapata kwa siku za karibuni.
Kupitia akauti yake ya Facebook, Bocco amekiri Azam imekuwa kimeo kwa siku za karibuni na kukiri kwamba watajirejkebisha na kubwa ni kuwamba radhi wote waliokwazwa na matokeo ya timu yao ambayo jioni ya leo iling;olewa rasmi kwenye michunoa ya Kombe la Mapinduzi kwa kucharazwa mabao 2-1 na Mafunzo ya Zanzibar.
Ujumbe wa Bocco ndio huu, usome mwenyewe;
"Napenda kuchukua nafasi hii kuwaomba radhi mashabiki wote wa Azam Fc kwa performance mbaya tulioonyesha kwenye mashindano ya Mapinduzi na mechi mbili za Ligi kabla ya kuja huku, matokeo ni sehemu ya mchezo inakubalika, lakin kitu kinacho angaliwa ni unapataje matokeo yawe mazuri au mabaya, tumepata matokeo mabaya kutoka kwenye performance mbaya zaidi kuwahi kuiona katika timu yetu tangu nilipoanza kucheza hadi sasa hivi, hivo tunawaomba radhi mashabiki wetu wote na kuwaaidi tutajituma na kupigania club yetu kwa moyo wetu wote."

Kadhalika naye Himid Mao aliomba radhi kama ujumbe wake unavyosomeka;
Napenda kuchukua nafasi hii kuwaomba radhi mashabiki wote wa Azam Fc kwa performance mbaya tulioonyesha kwenye mashindano ya Mapinduzi na mechi mbili za Ligi kabla ya kuja huku, matokeo ni sehemu ya mchezo inakubalika, lakin kitu kinacho angaliwa ni unapataje matokeo yawe mazuri au mabaya, tumepata matokeo mabaya kutoka kwenye performance mbaya zaidi kuwahi kuiona katika timu yetu tangu nilipoanza kucheza hadi sasa hivi, nasikia aibu sana tena zaidi ya sana sina njia ya kuelezea ni kiasi gani najiskia vibaya na aibu naa mini na wachezaji wenzangu wanajiskia vibaya kama nnavyo jiskia mimi.....
I will work as harder as i can to make things better for me & my team
Samahani kwa mara nyingine tena,
Usiku Mwema

No comments:

Post a Comment