STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 7, 2016

Yanga 2 Mtibwa 1, Henry Joseph alimwa red card

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2016/01/Yanga-vs-Mtibwa-znz-3.jpg
Mtibwa iliyolala kwa Yanga usiku huu
http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2016/01/Yanga-vs-Mtibwa-znz-2.jpg
Yanga iliyomaliza kazi Amaan dhidi ya Mtibwa Sugar
PAMBANO la Yanga na Mtibwa limeisha kwa matokeo ya 2-1, Yanga ikiibuka kidedea dhidi ya Wakata Miwa.
Yanga iliandika bao la pili na la ushindi lililofungwa na mtokea benchi Malimi Busungu aliyemalizia kazi nzuri ya Simon Msuva aliyepiga krosi murua iliyomkuta Busungu pekee yake na kupiga kichwa kilichompita kipa Said Mohammed.
Bao hilo lilifungwa dakika ya 82 na kuifanya Yanga kuongoza kundi B ikiwa na pointi 7 na Mtibwa kumaliza ya pili na pointi 4 na sasa wanasubiri kujua wanacheza na timu zipi kutoka kundi A ambapo Simba na JKU wataumana usiku wa kesho na mapema jioni, URA ya Uganda itakwaruzana na Jamhuri-Pemba.
Simba ndio inaoongoza kundi hilo kwa sasa ikiwa na pointi 4 ikifuatiwa na JKU kisha URA zote zikiwa na pointi 3 kila mmoja isipokuwa kutofautiana mabao ya kufungwa na kufunga, huku Jamhuri ikiburuza mkia ikiwa na pointi moja iliyotokana na sare dhidi ya Simba.

No comments:

Post a Comment