STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 8, 2016

MWANAUMEEEEEEEEEEEEEEEE NI MBWANA SAMATTA

 
http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/01/samatta-1.jpg
Add caption
MWANASOKA Bora wa Afrika kwa Wachezaji wa Ndani ni Mbwana Samatta, huku Yaya Toure MBWANA Samatta kila kona. Mwanasoka wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta usiku wa kuamkia leo ameweka rekodi ya kuwa Mwanasoka Bora wa Afrika kwa Wachezaji wa Ndani. Samatta amekuwa Mtanzania wa kwanza kunyakua tuzo hiyo baada ya kuwashinda Robert Kidiaba na Baghdad Bounedjah.
Hiyo ni tuzo ya pili kwa Samatta baada ya ile ya Mfungaji Bora wa Afrika akiwa ameisaidia klabu yake ya TP Mazembe kutwaa ubingwa wa Afrika mwaka 2015.
Klabu hiyo ya Mazembe ilishinda tuzo ya Klabu Bora Afrika, huku timu ya taifa ya Ivory Coast ikishinda tuzo Timu bora ya Afrika kwa wanaume na Cameroon ikishinda kwa upande wa wanawake.
Mfaransa Herve Renard, Kocha wa Ivory Coast alitwaa tuzo ya Kocha Bora wa Mwaka kwa mara ya pili baada ya mwaka 2012 kunyakua pia tuzo kama hiyo alipoisaidia Zambia kutwaa ubingwa wa Afrika na  kufikia rekodi ya  Bruno Metsu aliyenyakua mwaka 2001-2002
Mwanasoka Bora wa Afrika kwa mwaka 2015 ni Pierre-Emerick Aubameyang, akimpikua Yaya Toure wa Ivory Coast na Andre Ayew wa Ghana.

ORODHA KAMILI YA WASHINDI
MCHEZAJI BORA WA AFRIKA - Pierre-Emerick AUBAMEYANG (Gabon)
MCHEZAJI BORA ANAYECHEZA AFRIKA – Mbwana Aly SAMATTA
MCHEZAJI BORA WA KIKE - Gaelle ENGANAMOUIT (Cameroon)
MCHEZAJI BORA KIJANA - Victor OSIMHEN (Nigeria)
MCHEZAJI BORA ANAYECHIPUKIA VIZURI - Etebo Peter OGHENEKARO (Nigeria)
KOCHA BORA WA MWAKA- Herve RENARD (Ufaransa) – Kocha wa zamani wa Ivory Coast
REFA BORA WA MWAKA - Bakary Papa GASSAMA (Gambia)
TIMU BORA YA TAIFA – Ivory Coast
TIMU BORA YA TAIFA YA WANAWAKE- Cameroon
KLABU BORA YA MWAKA - TP Mazembe (DRC)
GWIJI WA AFRIKA - Charles Kumi GYAMFI (Ghana)
Samuel MBAPPE LEPPE (Cameroon)

KIKOSI BORA AFRIKA

Kipa: Robert Muteba KIDIABA (DRC)
Mabeki: Serge AURIER (Ivory Coast), Aymen ABDENNOUR (Tunisia), Mohamed MEFTAH (Algeria)
Viungo: Andre AYEW (Ghana), Yaya TOURE (Ivory Coast), Sadio MANE (Senegal), Yacine BRAHIMI (Algeria),    
Washambuliaji: Mbwana Aly SAMATTA (Tanzania), Pierre-Emerrick AUBAMEYANG (Gabon), Baghdad BOUNEDJAH (Algeria) 

WACHEZAJI WA AKIBA;

Djigui DIARRA (Mali)
Azubuike OKECHUKWU (Nigeria)
Kelechi NWAKALI (Nigeria)
Zinedine FERHAT (Algeria)
Adama TRAORE (Mali)
Victor OSIMHEN (Nigeria)

Kermit ERASMUS (Afrika Kusini)

No comments:

Post a Comment