
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 20 alijiunga na Dortmund kwa mkopo wa msimu mzima mwishoni wa Agosti mwaka jana, lakini amefanikiwa kuichezea timu hiyo mechi 12 pekee.
Kurejea kwa Januzaj Old Trafford kulifanywa rasmi jana na mkurugenzi wa michezo wa Dortmund amekiri kuwa kusitisha mkataba wa nyota huyo ni jambo bora kwa pande zote husika.
Mkurugenzi huyo amesema yalikuwa ni mapendekezo ya Januzaj mwenyewe kurejea United na uwepo wake Dortmund haukuwa na faida yeyote kwa klabu hiyo.
Man imemrejesha winga huyo kwa ajili ya kuimatrisha kikosi chake baada ya Kocha Louis Van Gaal kuuza wachezaji wake kadhaa nyota akiwamo Nani, Chicharito na Angel di Maria
No comments:
Post a Comment