STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 8, 2016

Claudio Makelele apewa shavu Monaco


http://img1.cfstatic.com/psg/claude-makelele_35549_wide.jpg
Claudio Makelele
KLABU ya Monaco ya Ufaransa, imemteua kiungo wa zamani wa Chelsea na Real Madrid, Claudio Makelele kuwa Mkurugenzi Mpya wa Ufundi. 
Klabu hiyo ilitangaza jana Alhamisi uteuzi wa nyota huyo wa zamani wa kimataifa wa Ufaransa, ikielezea kuwa, kibarua chake kikubwa kitakuwa ni kumsaidia Makamu wa Rais Vadim Vasilyev kuongoza upande wa michezo wa timu hiyo. 
Makelele alitimuliwa kibarua cha kuinoa Bastia Novemba 24, 2014 baada ya kufanya kazi kama Kocha Msaidizi katika klabu ya Paris Saint-Germain. Akihojiwa na mtandao wa klabu hiyo, Makelele amesema amefurahi kujiunga na klabu hiyo muhimu katika soka la Ufaransa na kuahidi kufanya bidii na kuisaidia timu hiyo.
Enzi za uchezaji wake, mkali huyo alikuwa akitawala dimba la kati kiasi cha kuwapa wakati mgumu wapinzani wake.
 

No comments:

Post a Comment