STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 8, 2016

Samatta sasa kina kona, anukia Nantes

KLABU ya Ligi Kuu ya Ufaransa, Ligue 1 ya Nantes inaripotiwa kuanza mazungumzo rasmi na wawakilishi wa Mbwana Samatta pamoja na klabu ya TP Mazembe. 
Klabu hiyo imedaiwa kuwa ina nia ya kupata saini ya Samatta katika kipindi hiki cha dirisha dogo la usajili ili iweze kumtumia kwa msimu uliobakia. 
Kwa mujibu wa mwakilishi wa Samatta, Nantes inataka kila kitu kimalizike kabla ya Januari 20. Nantes inamtaka Samatta ili kuimarisha safu yake ya ushambuliaji ambayo msimu huu inaonekana kuwa butu kwa kufunga mabao 14 pekee. 
Nantes inashikilia nafasi ya 13 katika msimamo wa ligi hiyo baada ya kucheza michezo 19 ikikusanya jumla ya pointi 24.
Timu hiyo Jumapili itashuka uwanjani kuvaana na St Entienne katika mfululizo wa ligi hiyo.

No comments:

Post a Comment