STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 8, 2016

Simba yaikwepa Yanga kiaina, kuvaana na Mtibwa

Mashabiki wa Simba wanaosubiri kuipa sapoti timu yao Jumapili jioni dhidi ya Mtibwa Sugar
BAO pekee la Jonas Mkude la dakika ya 65 limeiwezesha Simba kutinga nusu fainali na sasa itaavana na Mtibwa Sugar jioni ya Jumapili, ikikwepana kuvaana na Yanga iliyotangulia mapema tangu jana.
Kulikuwa na dalili za Simba kuvaana na Yanga kama matokeo yangeisha kwa sare ya 0-0, lakini bao la Mkude liliweka mambo sawa na sasa vijana wa Msimbazi watakuwa wakinoa makucha yao ili kuvaana na Mtibwa waliocheza nao fainali za mwaka jana na kuichapa kwa mikwaju ya penalti.
Yanga wenyewe itakuwa na kibarua dhidi ya URA ambayo mapema jioni ya leo ilipata ushindi wa baoa 1-0 dhidi ya Jamhuri.
Kama Yanga na Simba zitavuka hatua hiyo zitaumana Jumatano usiku kwenye fainali ikirejea fainali za mwaka 2011, ambazo Simba ilitwaa taji lake la pili kwa kuizabua Yanga mabao 2-0.

No comments:

Post a Comment