STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 7, 2016

Yanga, Mtibwa ngoma nzito Amaan

Mtibwa
Yanga
PAMBANO la timu za Mtibwa Sugar na Yanga bado ngoma nzito kwani mpaka sasa dakika chache kabla ya mapumziko, matokeo ni sare ya 1-1.
Mtibwa walikuwa wa kwanza kuandika bao dakika ya 10 kupitia kwa chipukizi, Shiza Kichuya akimalizia pasi na Vincent Barnabas kabla ya Yanga kuchomboa dakika ya 41 kwa mkwaju wa kiufundi uliofungwa na Issofou Boubacar baada ya Donald Ngoma kuchezewa vibaya na kuwa faulo ambapo Mniger huyo alimtungua kipa Said Mohammed 'Nduda'.
Kabla ya mabao hayo timu zote zilipoteza nafasi nyingi za wazi, huku Yanga ikionekana kuzinduka baada ya kutunguliwa kwa kipa wao Deogratius Munishi 'Dida' ambaye katika mechi sita za nyuma alikuwa hajaruhusu bao kabla ya Azam 'kumtengua udhu' katika sare ya 1-1.

No comments:

Post a Comment