STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 7, 2016

Nyota yaanza kumuwakia Samatta mapema...!

Mbwana Samatta (kushoto) alipokuwa akifanya majaribio CSKA Moscow
MANENO ya Wahenga huwa hayapotei. Wanasema dalili njema uanza asubuhi. Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta ameanza kuwakiwa taa ya kijani katika tuzo za Afrika baada ya kutajwa miongoni mwa nyota wa kikosi cha wachezaji 11 Bora wa Caf 2015.
Samatta yupo Nigeria muda huu kwa ajili ya tuzo za Wachezaji Bora wa Afrika 2015 Glo Africa Awards 2015 zinazofanyika katika mji wa Abuja ametajwa kwenye kikosi hicho akiwa na wakali wengine wa dunia akiwa Mfungaji kinara wa mabao wa Bundesliga, Pierre-Emerick Aubameyang.
Wengine waliopo kwenye kikosi hicho ni kipa Robert Kidiaba, Serge Aurier, Aymen Abdennour, Mohammed Meftah, Andre Ayew, Yaya Toure, Sadio Mane, Yacine Brahimi, Aubameyang na Baghdad Bounedjah.
Huenda kwa mara ya kwanza Tanzania tukaandika historia kwa mwanasoka huyo kunyakua tuzo ya Mwanasoka Bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani.

No comments:

Post a Comment