STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, July 1, 2012

Azam Marine yaleta meli ya kisasa, abiria kusafiri na magari yao

Kampuni za meli za Azam Marine, imeamua kufanya kweli ambapo hivi karibuni inatarajia kuzindua meli kubwa ya kisasa ambayo itawawezesha abiria wake kwenda na magari yao visiwani Zanzibar. Meneja Mkuu wa kampuni hiyo Hussein Mohammed Said, amesema Julai 15 mwaka huu meli hiyo yenye urefu wa mita 100 itazinduliwa. Mohamedi alisema shida ya usafiri itapungua kwa asilimia kubwa kutokana na meli hiyo kuwa na uwezo wa kubeba abiria 1500, Mizigo tani 500 na magari 200 ambapo abiria atakae jisikia kwenda na gari lake Zanzibar, Pemba au Dar es Salaam ataweza kufanya hivyo. Waziri Mwenye dhamana ya Mawasiliano na Miundombinu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Hamadi Masoud, alithibitisha kwamba ana taaarifa za ujio wa meli hiyo ambayo alisema kwa kiasi kikubwa itakuwa ni ya kutoa huduma tu na siyakutengeneza faida. Meli hiyo inauwezo wa kwenda kasi ya notkomail 20.
MELI HIYO INAVYOONEKANA NDANI NA NJE

No comments:

Post a Comment