STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, July 1, 2012

Okwi kupaa kwenda Parma ya Italia

MSHAMBULIAJI wa kutumaini wa kimataifa wa timu ya soka ya Simba, Emmanuel Okwi anatarajiwa kutua nchini Italia kwa ajili ya kufanyiwa majaribio katika klabu ya Parma inayoshiriki Ligi ya Seria A, baada ya kuzitosa ofa za timu za Afika Kusini. Mganda huyo ambaye amekuwa chachu kubwa ya Simba kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu msimu uliopita, anatarajiwa kwenda nchini humo, keshokutwa. Habari za kuaminika toka ndani ya Simba na kuthibitishwa na mmoja wa wajumbe wa kamati ya Utendaji aliyekataa kutajwa jina lake, zinasema kuwa Okwi anaenda huko kwa ajili ya kufanya mazungumzo na Parma. "Ni kweli Okwi anatarajiwa kutua Italia Julai 4 kwa ajili ya kufanya mazungumzo na klabu ya Seria A ya Parma kwa ajili ya kujiunga nao kwa msimu ujao baada ya kuachana na ofa za klabu za Orlando Pirates, Mamelodi Sundowns na Super Sports zilizokuwa zikimtaka," chanzo hicho kilidokeza. Chanzo hicho kilidokeza kuwa, iwapo Mganda huyo atafanikuwa kunyakuliwa na Parma huenda Simba ikavuna mamilioni ya fedha kwa usajili huo. Hata hivyo Simba italazimika kugawana mgao huo unaokadiriwa kufikia Sh Bilioni 2 na klabu ya Sc Villa ya Uganda iliyowauzia nyota huyo ambaye aliidhalilisha Yanga kwenye mechi ya kufungia msimu kwa kufunga mabao mawili na kusaidia jingine moja. Hiyo haitakuwa mara ya kwanza Simba kuuza wachezaji wake na kuvuna fedha, kwani mwaka jana iliwauza Mbwana Samatta na Patr
ick Ochan kwa TP Mazembe na kuvuna fedha za kutosha hiyo ni mbali na zile za akina Danny Mrwanda, Henry Joseph na wengineo.

No comments:

Post a Comment