STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, July 1, 2012

Yanga yatamba 'MTATUKOMA' safari hii

UONGOZI wa
klabu ya soka ya Yanga umetamka neno moja tu 'Mtatukoma' wakitambia kikosi chao katika ushiriki wao wa michuano ya Kombe la Kagame. Yanga watashiriki michuano hiyo itakayoanza Julai 14 na kumalizika mwishoni mwa mwezi huu kama mabingwa watetezi, michuano itakayofanyika kwenye ardhi ya Tanzania Bara. Afisa habari wa Yanga, Louis Sendeu alisema kwa namna kikosi chao kilivyoimarishwa na kujifua wana hakika ya kutetea taji hilo, na pia kufanya vema kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao. Sendeu, alisema kwa halili yoyote wapinzani wao watakaopambana kwenye michuano hiyo ya Kagame na Ligi Kuu wanapaswa kujipanga kwani vinginevyo watakiona cha moto. "Kwa kweli Watatukona kwa namna tunavyoendelea vema na maandalizi yetu ya michuano ya Kagame na kujipanga kwa Ligi Kuu msimu ujao kama unavyojua tumeshaanza kujifua na tumeimarisha kikosi kwa kunasa wachezaji kadhaa," alisema. Sendeu alisema, anaamini wachezaji wapya waliosajiliwa kwa ajili ya michuano hiyo na ligi ijayo wataisaidia Yanga kurejesha makali yake baada ya kumaliza msimu wakiambulia patupu wakipoteza ubingwa na kukosa hata nafasi ya kuiwakilisha nchini katika michuano ya kimataifa. Yanga ilimaliza ligi ikiwa nafasi ya tatu, ikiziacha Simba iliyotwaa ubingwa na Azam walioshika nafasi ya pili wakiwatambia na kupata fursa ya uwakilishi wa nchini katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho. Kikosi hicho cha Yanga kinaendelea kunolewa kwa sasa na Kocha Msaidizi ambaye ndiye Kaimu Kocha Mkuu, Fred Felix Minziro baada ya aliyekuwa kocha mkuu, Kostadin Papic kutimika kwao baada ya kutoongezewa mkataba mwingine na klabu hiyo. Tayari uongozi wa juu ya Yanga umesema wakati wowote utalitangaza jina la kocha mkuu wa timu hiyo baada ya kupitia maombi ya makocha bora watano waliopita katika orodha ndefu ingawa majina ya makocha hao haijawekwa bayana zaidi ya tetesi wapo wa ndani ya Afrika na Ulaya. Timu hiyo jana ilikitambulisha kikosi chake kwa mashabiki wa soka jijini Dar kwa kuumanana na Express ya Uganda na kuikandamiza mabao 2-1, mabao yote ya Yanga yakitupiwa nyavuni Jerry Tegete kwa pasi murua za kinda la Stars, Simon Msuvah na Bahanuzi.

No comments:

Post a Comment