STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, July 29, 2012

TPBO yasitisha mapambano kisa....!

ORGANAIZESHENI ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO), imesitisha kwa muda mapambano yao yote ya ngumi ili kupisha mfungo wa Mwezi wa Ramadhani. Rais wa TPBO, Yasin Abdallah 'Ustaadh' alisema wamechukua uamuzi huo ili kuwapa nafasi mabondia na mashabiki wa ngumi kujikita kwenye ibada hiyo ya funga ambayo ni moja ya nguzo tano na muhimu kwa maisha ya waumini wa dini ya Kiislam. Ustaadh, alisema kusitishwa kwa michezo hiyo haina maana kwamba TPBO haifanyi kazi, kisha akafafanua kuwa ofisi zao zinaendelea kufanya kazi kama kawaida isipokuwa haitaruhusu pambano lolote katika kipindi hiki cha mfungo. "TPBO, tumesimamisha mapambano yote ya ngumi ndani ya mwezi mtukufu wa Ramadhani ili kuungana na waislam katika utekelezaji wa ibada yao ya funga, ingawa ofisi zetu zilizopo Temeke Mwembeyanga zinaendelea kufanya kazi ikiratibu mapambano yatakayofanyika baada ya mfungo huo," alisema Ustaadh Yasin. Aidha, alisema TPBO inawatakia mfungo mwema mabondia na wadau wa ngumi wenye imani na dini ya Kiislam ili waweze kufunga na kumaliza bila matatizo. Mwisho

No comments:

Post a Comment