STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 30, 2012

Kipemba sasa vitani na Waanchari, Warenchoka

MUIGIZAJ
MUIGIZAJI mkongwe nchini, Issa Kipemba anajipanga kufyatua filamu mpya inaozungumzia uhasama wa makabila mawili makuu ya mkoani Mara ya Warenchoka na Waanchari. Nyota huyo wiki iliyopita alikuwa mkoani humo kuonana na 'machifu' wa koo hizo ili kujua chanzo vita vyao na pia kupata baraka za kuicheza filamu hiyo. Akizungumza na NIPASHE juzi siku moja baada ya kurejea toka safarini, Kipemba aliyewahi kutamba na Kaole Sanaa, alisema safari yake ilikuwa na mafanikio tofauti na alivyofikiri. Kipemba alisema amejifunza mengi katika safari yake hiyo na kwa sasa anajipanga ili kufyatua filamu hiyo itakayokuja baada ya kazi yake ya 'Injinia' kuingiza sokoni. Alisema hajajua filamu hiyo itawashirikisha wasanii wapi kutokana na ukweli inahitaji umakini wa hali ya juu kama alivyofanya katika kazi yake ambayo inakaribia kutoka hewani ya 'Injinia'. "Unajua sitaki kulipua kazi, nataka kuonyesha mfano kwa wadau wengine wa filamu, kwamba kazi hii si ya kulipuliwa kwa nia ya kujipatia fedha tu," alisema.

No comments:

Post a Comment