STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, May 5, 2014

Suarez ashinda tena tuzo England

http://thebeastbrief.com/wp-content/uploads/fbl-eng-pr-man_city-liverpool_yat6982_33846537.jpgNYOTA ya neema imeendelea kumuangazia Mshambuliaji mahiri wa klabu ya Liverpool, Luis Suarez baada ya kutajwa tena kuwa Mchezaji bora wa Mwaka wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo nchini Uingereza. 
Strika huyo kutoka Uruguay, aliyefunga mabao mabao 30 (kabla ya mechi ya usiku huu)msimu huu katika Ligi Kuu na kuiwezesha timu yake kufukuzia taji la ubingwa toka walipofanya hivyo mwaka 1990. 
Suarez, 27, alipata asilimia 52 ya kura zilizopigwa na waandishi hao akimshinda nahodha wake Steven Gerrard, huku Yaya Toure wa Manchester City akishika nafasi ya tatu. 
Mshambuliaji huyo hiyo ni tuzo ya pili baada ya wiki iliyopita alitajwa kama mchezaji bora na Chama cha wachezaji wa Kulipwa nchini humo (PFA) anatarajiwa kupokea zawadi yake hiyo katika sherehe za chakula cha usiku zitakazofanyika jijini London Mei 15.

No comments:

Post a Comment