STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, May 11, 2015

Carlo Ancelotti ajipa matumaini kwa Juventus

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/02921/ancelotti_2921770b.jpgMENEJA wa klabu ya Real Madrid, Carlo Ancelotti anaamini kikosi chake kinaweza kugeuza matokeo ya mabao 2-1 waliyochapwa na Juventus na kutinga hatua fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Pamoja na kutoka sare ya mabao 2-2 katika mchezo wa La Liga dhidi ya Valencia juzi. Mabingwa hao wa Ulaya sasa wako nyuma ya vinara Barcelona kwa alama nne huku kukiwa kumebaki michezo miwili katika ligi. 
Akihojiwa kocha Ancelotti amesema wanahitaji kuwa mawazo chanya na kuthamini jinsi walivyocheza vyema katika mchezo huo. 
Kocha huyo aliendelea kudai kuwa makosa madogo madogo ndio yaliyowagharimu, lakini wanahitaji kutulia na kujiandaa kwa ajili ya mchezo wao wa keshokutwa (Jumatano) dhidi ya Juventus.
Katika mfululizo wa michuano hiyo kesho Jumanne, Bayern Munich watakuwa nyumbani Alliaz Arena ikli kubadilisha matokeo ya mabao 3-0 iliyonyukwa katika mechi ya wiki iliyopita nchini Hispania.

No comments:

Post a Comment