STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, May 11, 2015

Mbeya City yawatunuku nyota wake, kocha Mwambusi

IMG-20150510-WA0010KLABU ya Mbeya City imewapa tuzo wachezaji wake pamoja na Kocha Juma Mwambusi kwa kuiwezesha timu hiyo kukamata nafasi ya nne katika Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2014-2015.
Tuzio hizo zilitolewa mara baada ya mchezo wao wa mwisho wa Ligi Kuu kati yao ya Polisi Moro ambapo Mbeya iliibuka washindi wa bao 1-0.
Kwenye tuzo hizo Kocha mkuu Juma Mwambusi alipata tuzo kama kocha mwenye mafanikio makubwa ndani ya kikosi cha city na ligi kwa ujumla Paul Nonga, Deus Kaseke, Themi Felix walipata tuzo ya heshima kwa kufanya vizuri misimu miwili  Rafael Alfa na Kenny Ally walipata tuzo ya  wachezaji chipukizi waliofanikiwa Haningtony Kalyusubula alipata tuzo ya  mlinda lango bora  na Juma Nyosso, Hassan Mwasapili na Peter Mwalyanzi walipata tuzo ya uchezaji bora
IMG-20150510-WA0009
Halikadhalika wachezaji wengine 18 nao walipata zawadi  ikumbukwe kuwa zawadi na tuzo hizo walizopata wachezaji wa City zimeambatana na bahasha iliyonona vizuri kutoka uongozi na mashabiki wa Mccfc.

IMG-20150510-WA0004
Hanington Kalyesubula akipokea tuzo

No comments:

Post a Comment