STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 15, 2015

Hapana! Ronaldo Kaongopa? Arukwa fedha za Nepal

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2015/02/08/256E0D7200000578-2944513-Ronaldo_looks_glum_after_being_left_on_the_turf_follow_a_challen-a-31_1423391475170.jpgSHIRIKA la Misaada la Save the Children limekanusha taarifa kuwa Cristiano Ronaldo ametoa msaada ya Euro Milioni 7 kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi nchini Nepal. 
Kauli ya shirika hilo imekuja kufuatia taarifa kuwa Ronaldo mwenye umri wa miaka 30 ametoa kiasi hicho cha fedha kwenda kusaidia waathirika wa tetemeko hilo. 
Katika taarifa ya shirika hilo imedai kuwa, Ronaldo akiwa Balozi wao amekuwa akipaza sauti kueleza matatizo wanayokutana nayo watoto duniani. 
Lakini taarifa hiyo iliendelea kudai kuwa ripoti za hivi karibuni kuwa Ronaldo ametoa fedha kwa shirika hilo la Save the Children kwa ajili ya waathirika wa Nepal sio za kweli. 
Zaidi wa watu 8,000 walifariki dunia kea tetemeko kubwa lililoikumba nchi hiyo Aprili 25 mwaka huu kabla ya lingine kutokea Mei 12 na kuua wengine karibu 110.

No comments:

Post a Comment