STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, May 11, 2015

Moyes anogewa La Liga, azipotezea klabu za EPL

http://img.thesun.co.uk/aidemitlum/archive/01727/moyes_1727193a.jpgAMENOGEWA! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya Meneja wa klabu ya Real Sociedad, David Moyes amezipasha klabu za Ligi Kuu zinazomuwinda kuwa hana mpango wa kwenda popote kufuatia tetesi kuwa atarejea nchini Uingereza. 
Kocha huyo raia wa Scotland alitimuliwa na Manchester United baada ya kuinoa katika kipindi cha miezi 10, Novemba mwaka jana kutokana na klabu hiyo kutofurahishwa na matokeo. 
Moyes alirejea tena uwanjani akiwa kocha wa klabu hiyo katika  mazingira ambayo alikuwa hana mazoea nayo katika Ligi Kuu ya Hispania. 
Wiki za karibuni kumezuka tetesi kuwa klabu za West Ham United na Newcastle United zimekuwa zikitaka saini yake, lakini mwenyewe amedai hana mpango wa kuondoka Hispania kwa sasa. 
Akihojiwa Moyes amesema kwa sasa anataka kuimarisha kikosi chake kwa ajili ya msimu ujao, jambo ambalo amefikia hatua nzuri hivyo hawezi kuacha mpaka azma yake itimie.

No comments:

Post a Comment