STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, August 15, 2013

News Alert; Sheikh Ponda aondolewa hospitali na kupelekwa Segerea?

HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa Katibu wa Taasisi na Jumuiya za Kiislam Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda amehamishwa toka hospitali ya Muhimbili alipokuwa amelazwa kupelekea gereza la Segerea.
Habari hizo zinasema askari Polisi wamefika hospitalini hapo na kuondoka na Sheikh Ponda ambaye jana alisomewa mashtaka akiwa kitandani.
Tunafuatilia kujua ukweli wa jambo hili sambamba na kujua kilichosababisha Sheikh huyo kukimbizwa huko wakati akiendelea kupata matibabu ya jehara alilolipata kwa kilichoelezwa kupigwa risasi na Polisi mjini Morogoro mwishoni mwa wiki wakai wa shamrashamra za sikukuu ya Eid el Fitry.

No comments:

Post a Comment