STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, August 15, 2013

Familia ya Sheikh Ponda yalaani kutolewa kwa sheikh huyoi hospitalini akiendelea na matibabu kupelekwa Segerea

Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu, Sheikh Ponda Issa Ponda (wa pili kulia), ambaye kwa sasa anakabiliwa na tuhuma za uchochezi,  akitolewa katika taasisi ya mifupa MOI, kuelekea katika gereza la Segerea jijini Dar es Salaam majira ya asubuhi leo. (Na Mpiga Picha Wetu)

DAR ES SALAAM, Tanzania

Kwa upande wao familia ya Sheikh Ponda wamesema wanalaani kitendo kilichofanywa na serikali cha kumuondoa ndugu yao hospitalini huku akiwa anaendelea kupata matibabu.

Msemaji wa familia hiyo Is-haq Rashid, alisema kutokana na hali hiyo kama familia wanalirudisha suala la Sheikh Ponda kwa uongozi wa jumuiya na Taasisi za kiislamu kwa ajili ya hatua zaidi ya kuhakikisha kiongozi mwenzao anakuwa salama.

“Uporaji huu wa mgonjwa unazidi kutupa mashaka juu ya dhamira ya serikali hasa ikiwa tunalituhumu jeshi la polisi katika kumdhuru Sheikh,hatujui kwanini kila wakati wanafanya mambo yao kwa kuvizia kama mwanzonui tuliwaomba viongozi wenzie wawe na subira juu ya yaliyotokea sasa tunaachia hili walizungumzie wao.”alisema Is-haq.


Wakati huo huo taarifa zilizopatikana zinaeleza kuwa viongozi wa jumuiya na taasisi za kiislamu jana walikuwa katika kikao kizito cha kujadili hatua hiyo ya kuporwa kwa Sheikh Ponda akiwa katika matibabu na kwamba leo watakutana na waandishi wa habari kuelezea msimamo wao.

No comments:

Post a Comment