STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, August 15, 2013

Timu ya Taifa ya Ngumi yakumbukwa kumwagiwa vifaa, fedha kesho Dar



TIMU ya taifa ya mchezo wa Ngumi iliyopo kambini ikijiandaa na ushiriki wa michuano ya kimataifa inatarajiwa kukabidhiwa vifaa vya michezo na nauli kwa wachezaji tuko litakalofanyika mchana wa leo jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT) vifaa na fedha hizo zinatolewa na Mkurugenzi wa  Shule za St Mary na Hoteli ya Kitalii iliyopo Bagamoyo, Rutta Rwakatare na ifanyika kwenye ofisi za BFT, jijini Dar.
Taarifa hiyo iliyosainiwa na Katibu Mkuu wa BFT, Makore Mashaga, inasema hafla hiyo itafanyika saa 6;30 ikiw na lengo la kuisaidia kamb ya mazoezi ya timu hiyo ambao inajiandaa na michuano ya Afrika itakayofanyika mezi ujao nchini Mauritius.
Uongozi wa BFT umedai umefurahishwa na kitendo hicho kinachotarajiwa kufanyika leo ukiwa umekuja wakati muafaka wakati timu hiyo ikihitaji msaada kwa sasa kwa maandalizi ya michuano hiyo na le ya mwakani ya Jumuiya ya Madola.
BFT ikatoa wito kwa wadau wengine wa michezo kujiokeza kuisaidia timu hiyo kwa madai ina hali mbaya kifedha.
"BFT tumefurahishwa mno na mwitikio wa Mkurugenzi huyo kwa kusikia na kuguswa kuhusu timu ya taifa ya ngumi na BFT, tunawaomba watanzania wengine wajitokeze zaidi kusaidia timu yetu ya taifa ili uwakilishi katika mashindano ya kimataifa uwe na tija," taarifa hiyo ya BFT inasomeka hivyo.
Pia BFT imeviomba vyombo mbalimbali vya habari kujitokeza kuhamasisha ili watanzania wengine kujitokeza kuendelea kusaida zaidi kwa madai msaada unahitajika wa vifaa vya mazoezi, matibabu, chakula, maji,nauli, nguo za mazoezi na posho za wachezaji.

No comments:

Post a Comment