STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 11, 2015

Hapa Javu, kule Bahanuzi, hivi mnatokaje kwa Mtibwa Sugar?

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhdEulqye6NB2gXsPi5nX52ruKNuZkwLExeKIBZx9YhfvRv9i-1GRUvXwcGWe-uVRRKZzgwsiMkZgmzbo80RFdgxlHnANAjRcCAnSAEfyBFFwRCrJPMxsv_FBRuFjUHKP11ERryy3d8XlE/s640/Javu.jpg
Hussein Javu
STRAIKA Hussein Javu, ameziangalia timu 15 zinazoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara inayoanza kesho Jumamosi. Kisha akakiangalia kikosi cha Mtibwa Sugar atakachokichezea msimu huu kwa mkopo akitokea Yanga ambacho kimesafiri mpaka Shinyanga ili kuanza msimu wa ligi dhidi ya Stand United, kisha akatabasamu huku akisema 'lazima heshima itarudi safari hii'.
Javu aliyesajiliwa na Yanga misimu miwili iliyopita akitokea Manungu, alisema kukutana kwake tena na Said Bahanuzi 'Spiderman' na wakali wengine ndani ya Mtibwa kumempa uhakika wa kurejesha heshima yake na ya klabu hiyo kwa mjumla katika ligi hiyo ya msimu huu.
Mtibwa iliyoanza kwa kasi katika ligi ya msimu uliopita kabla ya kutetereka, itaanzia mechi zake ugenini kabla ya kurudi Manungu kuzisubiri Ndanda na Majimaji kisha kuikaribisha Yanga katika pambano litakalochezwa Sept 30 kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.
"Kwa mziki huu uliopo Manungu, sioni wa kuizuia Mtibwa kurejesha heshima yake msimu huu, ni kazi pevu lakini tumejiandaa kufanya makubwa, hasa kutokana na kurudi nyumbani chini ya kocha Mecky Maxime," alisema Javu.
Javu, Bahanuzi ni baadhi ya wachezaji wapya nane waliotua kwa Wakata Miwa hao kwa ajili ya kuunda kikosi cha msimu huu cha Mtibwa Sugar chenye wachezaji 28, wakiwamo 20 waliokuwa msimu uliopita.
Wengine nane wapya ni kipa Hussen Sharrif 'Casillas' na Issa Rashid 'Baba Ubaya' ambao nao wamerudisha majeshi nyumbani wakitokea Simba.

No comments:

Post a Comment