STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 11, 2015

Lazima pachimbike Chanika, Ndonga zitapigwa hivi hivi!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEje2A78vXEe4Uo4cv-6s9mPx6Wq0Kif0wcoRpp930ZWk7OtAr3bMYet3LfivlK4JOjJVKxsPedLOpmffHtjd8sUlXJ6TL__ItbNw2pPa5ln6JBd4j88n55qMINxDsDLkfem7sagV3-nZwKR/s640/super+d+boxing+promotion.jpg
IWE isiwe ni lazima pachimbike Chanika, hii ni kutokana na mabondia Said Mbelwa na George Dimoso wanatarajiwa kupanda ulingoni ili kuzichapa katika pambano la kuwania Ubingwa wa Taifa wa ngumi za kulipwa.
Mabondia hao watazichapa siku ya Septemba 26 kwenye Ukumbi wa Butiama Villa Club, Chanika ambapo siku hiyo mashabiki wa soka hasa wa Simba na Yanga watakuwa wameshafahamukitu gani walichovuna kwenye pambano lao la  watani litakalofanyika kwenye Uwanja wa Taifa katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu wa 2015-2016.
Mratibu wa pambano hilo, Rajabu Mhamila 'Super D', alisema kuwa Mbelwa na Dimoso ambao tayari wapo kwenye kambi zao za maandalizi huku wakitambiana watazipiga katika pigano la raundi 10.
Super D alisema pambano hilo la uzito wa kati litasindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi likiliwemo la Seleman Zugo dhidi ya  Abdallah Luanje, Adam Ngange atakayeumana na Shaaban Mtengela.
Siku hiyo pia Said Uwezo ataonyesha uwezo wake dhidi ya Hassan Mgosi, Hamza Mchanjo yeye ataumana na Ally Maiyo katika mipambano tofauti isiyo ya ubingwa.
Super D alisema siku hiyo kutakuwa na uuzwaji wa DVD mpya za michezo kadhaa ya ngumi za kimataifa likiwamo pambano lililofunika mwaka huu wa 2015 kati ya Manny Pacquiao na Floyd Mayweather ambalo liliisha kwa Mmarekani Money Man kumchapa Man Pac

No comments:

Post a Comment