STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 16, 2014

Liverpool yawachinja Mashetani Wekundu Old Trafford

Steven Gerrard
KOCHA David Moyes ameendelea kuvunja rekodi za Manchester Utd baada ya Liverpool kupata penati mbili kwenye uwanja wa Old Trafford na kuifumua Mashetani Wekundu kwa mabao 3-0 katika mfululizo wa Ligi Kuu ya England na kuchupa hadi nafasi ya pili.
Penati hizo za vipindi viwili vimeifanya Manchester Utd kubaki kwenye nafasi ya 7 ikiwa na pointi 48 na Liverpool kufikisha pointi 62 na kuiengua Manchester City yenye pointi 60.
Mikkwaju miwili ya penati ya dakika ya 34 ya kipindi na jingine la dakika ya 46 kupitia nahodha Steve Gerrard na bao jingine la dakika ya 84 la Luiz Suarez lilitosha kumnyamazisha Moyes na vijana wake nyumbani kwa mara nyingine.
Penati ya kwanza ilitokana na Raphael da Silva kuunawa mpira  kabla ya Phil Jones alimvamia na kumuangusha Joe Allen wa Liverpool na kumsukuma na penati hiyo kumwamisha dakika moja baada ya kuanza kwa kipindi cha pili.
Liverpool ilipata penati nyingine ya tatu na Gerrard lakini mkwaju wake ukagonga mwamba na kurejea uwanjani kabla ya Luiz kuja kumalizia shuti la Daniel Sturridge baada ya kuzamisha bao la tatu lililoipa Liverpool ushindi mnono kuelekea kwenye mbio za ubingwa wa England.
Dakika chache baadaye  Arsenal itakuwa uwanja wa White Hartlane kuumana na mahasimu wao wa London Kaskazini, Tottenham Hotspur.

No comments:

Post a Comment