STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 16, 2014

Arsenal yaibutua Spurs yaendelea kuibana Liver

Arsenal's Tomas Rosicky after scoring against Tottenham
Kitu! Arsenal ikijipatia bao pekee lililowarejesha kwenye nafasi ya tatu


BAO la dakika ya pili lililofungwa na Romas Rosicky liliiwezesha Arsenal kuibuka na ushindi muhimu ugenini dhidi ya Tottenham Hotspur na kuendelea kufufua matumaini ya kumaliza ukame wa mataji iliyonayo kwa muda mrefu.
Tottenham ambayo imetoka kuchezea kichapo cha aibu cha mabao 3-1 katikati ya wiki kwenye Ligi ya Europa dhidi ya Benfica, licha ya kucharuka kusaka bao la kusawazisha walijikuta wakimaliza dakika 45 za kwanza wakiwa nyuma.
Hata pamoja na kufanya mabadiliko ya wachezaji, Spurs ilishindwa kulipa kisasi kwa wapinzani wao waliowafunga pia katika mechi ya mkono wa kwanza walipowafuata Emirates na kujikuta wakiendelea kusalia kwenye nafasi ya tano wakiwa na pointi 53, huku Arsenal ikichupa hadi nafasi ya tatu nyuma ya Liverpool ilitoka kuitoa nishai Manchester Utd ikiwa kwao.
Timu hizo mbili zina pointi 62 ila zinatofautiana mabao ya kufungwa na kufungwa nyuma ya Chelsea wanaoongoza wakiwa na pointi 66, Manchester City walikuwa wakishika nafasi ya pili mpaka mchana wa leo imerejea kwenye nafasi yake ya nne ikiwa na pointi 60.

No comments:

Post a Comment