STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, April 23, 2014

PSG yabakisha pointi tatu kutetea taji Ufaransa

MABINGWA watetezi wa Ligi ya Ufaransa (Ligue 1) PSG usiku huu imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Evian TG na kujiweka katika nafasi nzuri ya kutetea taji hilo ikibakisha pointi tatu
Bao pekee lililowekwa kimiani na Blaise Mataudi dakika moja kabla ya pambano hilo kwisha lilitosha kuwa ushindi muhimu kaioka pambano hilo lililoshuhudia wageni wa PSG wakicheza pungufu.
Beki Kassim Abdallah wa Evian alilimwa kadi ya njano ya pili dakika ya 61 na kusindikizwa na nyekundu na kuacha pengo kwa timu yake iliyoelekea kuikomalia wenyeji wao kabnla ya Mataudi kufunga bao hilo na kuifanya PSG kufikisha jumla ya pointi 82, 10 zaidi ya Monaco yenye 72.
Timu zote zimecheza michezo 34 na kukasaliwa na mechi nne kila moja kufungia msimu ambapo ushindi wa mechi moja kati ya hizo tatu utaipa nafasi PSG kutete taji hilo kwa mara ya pili mfululizo.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo iliyochezwa pia leo, Toulouse ikiwa nyumbani ililazimishwa suluhu ya 0-0 dhidi ya wageni wao Olympique Lyon

No comments:

Post a Comment