STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 24, 2014

Real Madrid yaizima Bayern Munich, ila kazi wanayo ugenini

Benzema (9) akishangiulia bao lake pekee lililoizamisha Bayern Munich
MABINGWA watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Bayern Munich imekubali kichapo cha bao 1-0 toka kwa wenyeji wao Real Madrid katika mechi ya mkondo wa kwanza ya Nusu fainali ya pili ya michuano hiyo iliyochezwa usiku wa kuamkia leo mjini Madrid -Hispania.
Baoa pekee la dakika ya 19 ya mchezo lililotumbukizwa kimiani na Karim Benzema lililitosha kuwapa wenyeji ushindi huo mwembamba kwenye uwanja wa Santiago Bernabeu.
Katika mchezo huo ilishuhudiwa wachezaji ghali wa klabu ya Real Madrid wanaodaiwa kuwa wagonjwa kupishana katika kipindi cha pili na kuwapa faraja vijana wa Carlo Ancelotte kupumua kabla ya wiki ijayo kurudiana na Wajerumani hao waliopoteza bafasi kadhaa za kufunga katika mechi hiyo.
Real Madfrid itakabiliwa na kazi nzito katika mchezo wa marudiano ili kulinda ushindi huo na kuvuta unyonge wa kutolewa mara katika hatua hiyo na wapinzani wao hao.

No comments:

Post a Comment