STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 24, 2014

Kivumbi Europa League kutimka leo Juve yaifuata Benfica

Juve itavuna nini leo Ureno
KIVUMBI cha Nusu Fainali  ya Ligi Ndogo ya Ulaya (UEFA Europa League) kinatarajiwa kutimka usiku wa leo wakati timu nne zilizotinga hatua hiyozitakapopepetana kwenye viwaja viwili tofauti.
Klabu za Sevilla na Valencia zote kutokea Hispania zilizopangwa kucheza pamoja zitakutana kwa mara ya kwanza katika hatua hiyo, wakati mabingwa wa Italia Juventus watakwaruzana na Benfica ya Ureno katika mechi zinazotarajia kuwa na msisimko wa aina yake.
Valencia na Sevilla ambazo zilipindua matokeo yao ya awali walipolazwa ugenini na kushinda nyumbani kwa idadi kubwa ya mabao dhidi ya Porto na Basel zinakutana kwa mara ya kwanza kwenye michuano ya Ulaya.Mechi za mkondo wa kwanza baina ya timu hizo mbili itaanziua nyumbani kwa Sevilla kabla ya wiki ijayo kuwafuata wapinzani wao hao.
Timu zote mbili zimewahi kunyakua taji hilo kwa vipindi tofauti, Sevilla mara mbili mfululizo mwaka 2006 na 2007 na wenzao walitangulia mwaka 2004.
Juventus itakayokuwa ugenini ilishawahi kunyakua taji hilo mara tatu mwaka 1977, 1990 na 1993 na ingependa kufanya kweli katia michuano ya mwaka huu baada ya ndoto zao na kutamba Ligi ya Mabingwa Ulaya kukwama na kutolewa kwenye hatua ya 16 Bora.
Waitalia hao wanaoelekea kutetea taji lao la Seria watakutana na Benfica ambao hawajawahi kunyakua taji hilo la Europa, ingawa mkononi tayari wana taji la ligi kuu ya nchi yao ya Ureno.
Ikitamba na nyota wake kama Carlos Tevez, Andre Pirlo, Paul Pogba na wengine Juventus itahitaji ushindi ugenini ili mchi yao ya marudiano wilki ijayo iwe nyepesi ingawa watarajie kupata upinzani mkali kwa mabingwa hao wa Ureno inayotambia wakali wake kama Lima kutoka Brazil., Rodrigo, Cordozo, na Andre Gomes

No comments:

Post a Comment