STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 24, 2014

Bomu jingine lalipuka Kenya

MATUKIO  ya kigaidi yamekua yakichukua vichwa vya habari mara nyingi nchini Kenya hasa baada ya nchi hiyo kupeleka wanajeshi wake nchini Somalia kupambana na wanamgambo wa kikundi cha kigaidi cha Al Shabaab.
Saa tatu na nusu usiku wa April 23 2014  bomu jingine limelipuka ndani ya gari karibu na kituo cha Polisi Nairobi.
Waziri wa mambo ya ndani amethibitisha kwa kusema Polisi wawili wamepoteza maisha kati ya watu wanne ambao wameuwawa huku hao wengine wawili wakihofiwa kuwa ni Mahabusu waliokuwemo kwenye gari hilo na Polisi.

No comments:

Post a Comment