STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 2, 2014

Bonite Bottlers wagawa runinga kwa wateja wao

KAMPUNI ya vinywaji baridi ya Bonite Bottlers Ltd jana ilikabidhi zawadi za luninga mpya za kisasa aina ya Sony LED zenye upana wa inchi 32 kwa washindi 29 wa shindano la Jionee Mwenyewe Kombe la FIFA la Dunia.
Katika promosheni hiyo iliyozinduliwa mapema mwezi uliopita, Coca-Cola itapeleka Watanzania 14 kwenda kushuhudia mechi ya robo fainali ya Kombe la FIFA la Dunia nchini Brazil mwezi Julai. Vile vile Coca-Cola itatoa mipira 8,000 yenye nembo ya FIFA World Cup na fulana 30,000.
Waliobahatika kushinda luninga na kukabidhiwa zawadi zao jana ni Paulina Mushi, Gabriel Warance (mwanafunzi), Moun Johnson (IT Technician), Rispa Waziri, Sophia Paulo, Abela Solomon, Chediel G. Mziray, Asha Ramadhan, Godfrey Mollel na Jackson Shayo (wafanyabiashara) na Simon Mrema (mchimba madini).
Washindi wengine ni Faidha Elidaima, Costantine Urio, Magreth Mshana, Enna Mbwambo, Emmanuel Tarimo, Julius Kimaro, Amir Ali, Emmanuel Mwasha, Gerald Swai, Joseph Mushi na Martine Temu wakazi wa mji wa Moshi.
Akizungumzia ushindi wake Gabriel Warance ambaye ni mwanafunzi jijini Arusha alishukuru Mungu kwa kumuwezesha kushinda luninga. Vile vile aliishukuru kampuni ya Bonite kwa kuleta promosheni hiyo ambayo imewawezesha wale watakaobahatika kushinda kubadili maisha yao kwa namna fulani.
Washindi wengine pia hawakusita kuonyesha furaha yao na kusema kwamba wataendelea kushiriki kwa lengo la kuendelea kushinda zawadi zaidi. “Hii ni nyota njema kwangu na naamini Mungu aliyeniwezesha kushinda zawadi hii ana uwezo wa kunipa tiketi ya kwenda Brazil kushuhudia 'laivu' fainali za Kombe la FIFA la Dunia,” alisema Godfrey Mollel ambaye ni mfanyabihashara.
Akizungumza baada ya kukabidhi zawadi kwa washindi, Meneja Mkuu wa Mauzo wa Bonite Bottlers, Christopher Loiruk aliwashukuru wateja wa Coca-Cola na wananchi kwa ujumla kwa kuendelea kuburudika na vinywaji vya Coca-Cola.
“Kombe la FIFA la Dunia ndiyo mchezo wenye mashabiki wengi zaidi duniani. Kwa kushirikisha wateja wetu katika promosheni hii, Coca-Cola itawawezesha mashabiki wa soka nchini Tanzania kuungana na wengine duniani kote kusherehekea kwa pamoja burudani ya Kombe la Dunia 2014,” anasema Loiruk
Washindi wamepatikana kwa kunywa vinywaji vya Coca-Cola na kupata vizibo viwili vyenye kutengeneza neno Brazil pamoja na kizibo cha ushindi. Kizibo cha ushindi kina picha ya kitu ambacho mteja ameshinda (TV, mpira au fulana) wakati kizibo cha ushindi wa zawadi ya tiketi kina nembo ya ndege kikiashiria safari ya kwenda Brazili kushuhudia moja kwa moja mechi ya Kombe la Dunia.

No comments:

Post a Comment