STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 10, 2015

Turan ajifunga miaka mitano Barcelona

http://static.sportskeeda.com/wp-content/uploads/2014/02/arda_turan-2116949.jpgKIUNGO wa kimataifa wa Uturuki, Arda Turan amekamilisha usajili wake katika klabu ya Barcelona baada ya kutia saini katika mkataba wa miaka mitano leo. 
Barcelona walikubali kutoa kitita cha Euro Milioni 41 kwa Atletico Madrid kw ajili ya nyota huyo wiki iliyopita. 
Hata hivyo, Turan amesisitiza hana shaka kuhusu uwezekano wa kurejea Atletico kwa muda mpaka Januari pindi Barcelona watakaporuhusiwa kumtumia. Kwa sasa Barcelona wanatumikia adhabu ya kutosajili kwa msimu miwili baada ya kukutwa na hatia ya kukiuka Sheria za Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kwa kusajili wachezaji walio chini ya umri wa miaka 18 kinyume cha sheria, adhabu ambayo inaishia Januari mwakani. Mkali huyo ametua akitegemewa kuziba pengo lililoachwa na Xavi aliyekimbilia Umangani.

No comments:

Post a Comment