STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 10, 2015

Jordan Henderson rasmi nahodha wa Liverpool, amrithi Gerrard

http://i1.liverpoolecho.co.uk/incoming/article8381445.ece/ALTERNATES/s1227b/Gerrard-Henderson.jpg
Nakukabidhi mikoba, usiniangushe!
WAKATI ikiendelea kumbembeleza nyota wake Raheem Sterling asalie klabuni, Liverpool, imethibitisha Jordan Henderson kuwa nahodha mpya wa timu hiyo akichukua nafasi ya Steven Gerrard aliyeondoka mwishoni mwa msimu uliopita. 
Henderson ambaye amesaini mkataba mpya Aprili mwaka huu, ndio aliyekuwa akipewa nafasi kubwa ya kupewa beji hiyo baada ya Gerrard kuhamia katika klabu ya Los Angeles Galaxy ya Marekani. 
Akihojiwa Henderson amesema siku zote amekuwa akitaka majukumu zaidi hususani katika kipindi hiki cha soka lake. 
Nyota huyo aliendelea kudai kuwa anajiona amekuwa kwasasa na yuko tayari kwa majukumu hayo kwani amejifunza mengi kutoka Gerrard katika kipindi chote ambacho chini yake.

No comments:

Post a Comment