STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 10, 2015

Azam yaenda Tanga kutambulisha nyota wake

https://thumbp22-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AL92imIAABY%2FVZ%2BaswTxoL0v9NM&midoffset=2_0_0_1_4179536&partid=11&f=1214&fid=Inbox&m=ThumbnailService&w=3000&h=3000
Wachezaji wakijiandaa na safari kuelekea Tanga
https://thumbp22-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AL92imIAABY%2FVZ%2BaswTxoL0v9NM&midoffset=2_0_0_1_4179536&partid=4&f=1214&fid=Inbox&m=ThumbnailService&w=3000&h=3000
Usiniangushe Migi
https://thumbp22-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AL92imIAABY%2FVZ%2BaswTxoL0v9NM&midoffset=2_0_0_1_4179536&partid=5&f=1214&fid=Inbox&m=ThumbnailService&w=3000&h=3000
Muingereza mwenyewe huyu hapa
https://thumbp22-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AL92imIAABY%2FVZ%2BaswTxoL0v9NM&midoffset=2_0_0_1_4179536&partid=7&f=1214&fid=Inbox&m=ThumbnailService&w=3000&h=3000
Migi akipasha na wenzake mapema leo

KLABU ya Azam ikiwa na nyota kadhaa wa kimataifa akiwamo Jean Baptiste Mugiraneza 'Migi'na Muingereza Ryan Burge imeondoka jijini kuelekea Tanga tayari kwa mechi mbili za kujipima nguvu kujiandaa na Kombe la Kagame litakaloanza wiki ijayo jijini Dar es Salaam.
Azam iliyofanya mazoezi mapema leo asubuhi itashuka dimba la Mkwakwani, Tanga kesho kuumana na Africans Sports kabla ya Jumapili kupepetana na Wagosi wa Kaya kwa mechi ya pili, kisha kurudi Dar kusubiri mechi zake za kundi C katika michuano hiyo ya Kagame itakayomaliza Agosti 2.
Mabingwa wa zamani wa Tanzania wanaenda kunoa makali kabla ya kuja kufanya kweli Dar katika Kagame ambayo inashirikisha timu 13 na Azam imepangwa kundi moja na KCCA ya Uganda, Al Malakia ya Sudan Kusini na Adama City ya Ethiopia.
Katika mechi hizo za wikiendi, Azam itatambulisha nyota wake wapya akiwamo Migi na Burge ambao wapo hatua ya mwisho kutua kwa Matajiri hao wa Tanzania.

No comments:

Post a Comment