STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 10, 2015

Yohan Cabaye arejea England, aitosa PSG

http://e2.365dm.com/14/02/768x432/Yohan-Cabaye-Paris-St-Germain_3076500.jpg?20140201152736
Yohan Cabaye
KIUNGO fundi wa zamani wa Newcastle United, Yohan Cabaye amerejea Ligi Kuu ya England kutoka Ligue 1 ya Ufaransa.
Kiungo huyo amemwaga wino wa kukipiga klabu ya Crystal Palace akitokea PSG ya Ufaransa na kumfanya aungane tena na kocha wake, Alan Pardew. 
Klabu ya Crystal Palace imethibitisha kumsajili kiungo huyo wa kimataifa wa Ufaransa kwa mkataba wa miaka mitatu. 
Inaaminika kuwa Palace imelipa ada ya Pauni milioni 10 kwa ajili ya kumnasa kiungo huyo aliyefanya kazi na Pardew kwa miaka mitatu wakati kocha na yeye wakiwa katika klabu ya Newcastle United. Kipindi akiichezea timu hiyo, Cabaye alikuwa akihesabiwa kama mmoja wa viungo bora katika Ligi Kuu. Kiwango chake hicho ndio kilichangia kwa kiasi kikubwa kuwafanya PSG kutoa karibu pauni milioni 20 kumsajili mapema mwaka jana.

No comments:

Post a Comment