
Hata hivyo, Van Gaal alikataa kuzungumza lolote kuhusu habari za kuuzwa kwa Mholanzi mwenzake Robin van Persie kwa Klabu ya Uturuki Fenerbahce.
Akijibu swali kuhusu kuuzwa kwa Van Persie, Van Gaal alisema: "Tukihisi anapaswa kwenda, utasikia toka Manchester United. Kwa sasa bado."
Alipohojiwa kuhusu mipango yao ya Uhamisho na kama inakwenda kama walivyotarajia, Van Gaal alikataa kusema kwa undani na badala yake kueleza: "Huwezi kujibu hilo kwani kununua na kuuza ni kitu kinachoendelea na hatujafika mwisho wake. Mwisho ni Agosti 31. Hatuwezi kusema lolote kuhusu Uhamisho wetu, mikakati yetu kwani nyie mtaandika kila kitu."
Aliongeza: " Manchester United haiwezi kununua kwa sababu ya kununua tu. Ukinunua lazima iwe ni kitu bora kuliko ulichonacho."

Depay aliongea: "Hii ni Klabu kubwa Duniani na hivyo ni lazima nicheze kwa ajili ya Vikombe. Nimekuja kushinda Vikombe."

Alipoulizwa kuhusu kufanana na Cristiano Ronaldo aliejiunga Man United akiwa na Miaka 18, Depay alieleza: "Sitaki kujifananisha na Mtu kama yeye. Cristiano Ronaldo ni mmoja wa Wachezaji bora Duniani na sitaki kusema sana, nitaachia Miguu yangu iongee!"
No comments:
Post a Comment