STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 22, 2013

Shasta ahairisha kugawa utamu wa penzi

http://thumbp4-ne1.thumb.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=ACbkimIAAAlPUdQbXwAAAJWB87w&midoffset=2_0_0_1_35347&partid=2&f=1215&fid=Inbox&w=480&h=297
Shasta akiwa katika pozi nyumbani kwake

MSANII wa filamu aliyejitosa pia katika muziki, Leah Mussa 'Shasta' amesitisha kwa muda harakati za kusambaza wimbo wake uitwao 'Utamu wa Penzi' ili kupisha mwezi mtukufu wa Ramadhani, imeelezwa.
Akizungumza mwishoni mwa wiki, Shasta alisema kuwa wimbo huo alioimba na H-Mbizo umeshakamilika na kilichobaki ni mambo madogo tu na kwamba, baada ya kumalizika kwa mfungo na sikukuu ya Idd ataendelea na kazi ya kuusambaza.
"Sasa wimbo huu utatoka baada ya Sikukuu ya Idd El Fitri," alisema Shasta ambaye amejitosa katika muziki baada ya kuvutiwa na wimbo 'Majanga' wa shoga yake na msanii mwenzake katika  filamu, Snura Mushi.
Baadhi ya filamu alizoshiriki Shasta ni 'Ong'wana', 'Julia', 'Kisasi za Mzimu', 'Siri za Majini' na 'Deception'.

No comments:

Post a Comment