STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 22, 2013

TMK Wanaume Family Sasa Tufurahie


KUNDI la muziki wa kizazi kipya la TMK Wanaume Family 'Mapanga Shaa', linatarajiwa kuuachia hewani wimbo wao mpya uitwao 'Tufurahie'.
Wimbo huo uliokamilika wiki iliyopita ni kati ya kazi mpya za kundi hilo baada ya kutamba na 'Kichwa Kinauma' na 'Tutaonekanaje'.
Akizungumza na MICHARAZO, Meneja wa TMK, Said Fella alisema wimbo huo ulirekodiwa katika studio za Tuddy Thomas wa Ngoma Records na utaachiwa leo Jumatatu.
Fella alisema katika wimbo huo, kazi kubwa imefanywa na YP, Mheshimiwa Temba na Said Chegge, na kwamba wanatumai utafanya vizuri kama ilivyokuwa kwa nyimbo zao nyingine.
"Umeandaliwa vizuri na hivyo tunaamini kwamba nao utatamba," alisema Fella.
Katika hatua nyingine, Fella alisema video ya wimbo wa msanii Is'haka Aslay 'Dogo Aslay' uitwao 'Bado Mdogo' alioimba kwa kushirikiana na Linnah wa THT imekalimika.
Wimbo huo umeelezewa na Dogo Aslay kuwa ni kisa cha kweli, akidai kwamba yupo mama mwenye umri mkubwa aliyekuwa akimghasi kwa kumtaka kimapenzi licha ya yeye kumkatalia kwa kumwambia kuwa yeye (Aslay) bado mdogo na hivyo asingependa kujihusisha na masuala hayo ya mapenzi.

No comments:

Post a Comment