STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 22, 2013

Mwakyembe, Maugo kupaa kesho kwenda Russia

Mada Maugo

Benson Mwakyembe (kushoto)
MABONDIA watanzania wanaocheza ngumi za kulipwa, Mada Maugo 'King Maugo Jr' na Benson Mwakyembe wanatarajia kuondoka nchini kesho (Jumanne) kuelekea Russia kwa ajili michezo yao ya kimataifa dhidi ya wenyeji wao.
Wanamasumbwi hao wataondoka majira ya saa 10 jioni na watapanda ulingoni Jumamosi ya wiki hii katika mipambano yao ya uzito wa kati wa Kilo 75 (Super Middle).
Rais wa TPBO-Limited, Yasin Abdallah 'Ustaadh', aliiambia MICHARAZO kuwa, Maugo yeye ataenda kupigana na Movsur Yusupov  wakati Mwakyembe ataonyeshana kazi na Apti Ustarkhanov kwenye michezo itakayochezwa kwenye ukumbi wa Trade &Intertainment uliopo mjini Kasiysk, nchini Russia.
Ustaadh alisema mapambano yote hayo yatakuwa na raundi 8 kila mmoja na kwamba Watanzania hao wataungana na wakala wao kutoka Kenya, Thomas Mutua katika mji wa Dubai.
Rais huyo wa TPBO alisema mpinzani wa Maugo rekodi yake inaonyesha amecheza mapambano matatu na yote ameshindwa moja likiwa kwa KO wakati mpinzani wa Mwakyemba amecheza mechi mbili na kushinda moja na kuchapwa moja.
Hata hivyo, alisema pamoja na rekodi hizo zisizovutia kwa wapinzani wao, bado Maugo na Mwakyembe wanapaswa kwenda nchini humo na tahadhari kubwa kwani Warusi huwa hawaruhusu mabondia wa ngumi za kulipwa kucheza mpaka wawe wamepitia ngumi za ridhaa na kushiriki michezo ya Olimpiki.
Akizungumza safari hiyo, Mwakyembe aliiambia MICHARAZO asubuhi hii kwamba licha ya kutomfahamu vyema mpinzani wake, lakini anawaahidi Watanzania kwenda kuwawakilisha vyema katika mchezo huo wa kimataifa ambao ni wa pili kwake nje ya nchi.
"Naahidi sintowaangusha watanzania katika mechi hiyo ya Jumamosi, naenda nikiwa na imani ya kutaka kuweka rekodi kwa kumtwanga mwenyeji wangu na kurejea nchini kwa heshima zote, najiamini kwa mazoezi niliyofanya," alisema.
Kuhusu safari hiyo, Mwakyembe alisema kila kitu kimekaa vyema na kwamba panapo majaliwa ataondoka na mwenzake (Mada Maugo) kesho saa 10 jioni.

No comments:

Post a Comment