STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 22, 2013

Mwili wa Mr Bomba kuagwa muda huu Muhimbili rariba kamili hiko hivi

REV. John Makanyagana
Msanii John Makanyaga enzi za uhai wake
MWILI wa muigizaji mkongwe nchini, Mchungaji John Makanyaga unatarajiwa kuagwa asubuhi hii katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kabla ya saa 8 kufanyiwa misa kwenye Kanisa la Anglicana tayari kwa ajili ya kusafirishwa kwenye kuzikwa kwao Mpwapwa.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa hivi punde na Adam Malele' Swebe', mmoja wa waigizaji wenzake wa zamani wa Kaole Sanaa Group, mwili wa msanii hiyo aliyefahamika zaidi kama Mr Bomba utafanyiwa misa ya maombezi kanisa la Ilala Sharifu Shamba
Swebe alisema baada ya ibada hiyo ya mazishi kanisani hapo, mwili huo utasafirishwa kwenda Mpwapwa Dodoma kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika kesho Jumanne.
Marehemu Mr Bomba alifariki juzi hospitali ya Muhimbi kwa tatizo la uvimbe wa kansa katika ini na enzi za uhai wake alitamba na tamthilia mbalimbali kupitia kituo cha ITV kabla ya kuhamia kwenye filamu.
Pia alikuwa ni mwalimu na Mcghungaji wa kanisa la Anglakana mpaka mauti yalipomkumba, ambapo yamekuja huku watanzania wakiendelea kuuguza machungu ya vifo vya wasanii wengine wa uigizaji na muziki vilivyotokea mfululizo tangu mwaka jana.

No comments:

Post a Comment